The Land Transport Regulatory Authority (LATRA)
Dar-es-salaam, Tanzania
Posted 2 days ago
Mwenyeji Wako Ukija Pemba
Ofisi ya Mufti inatoa huduma kwa jamii, huduma zinazotolewa ni Usajili wa Misikiti, Madrasa, Kusilimisha wasiokua waislamu, Kuendesha mafunzo ya ndoa, kutoa fatwa katika mambo mbalimbali ya kiislamu na kusuluhisha migogogoro ya ndoa.
Utaratibu wa Usajili wa Misikiti/Madrasa
Kabla ya kufika Ofisi ya Mufti, muhusika anatakiwa kwanza aandike barua yake yenye kichwa cha habari ya ombi la kusajili Msikiti/Madrsa.
Katika barua hiyo anatakiwa aeleze habari zote muhimu zinazo jitosheleza na ombi lake la Msikiti/Madrasa
USAJILI WA MISIKITI
Katika ombi la usajili wa Misikiti Mteja anatakiwa ataje jina la msikiti wake, pahala ulipo, Shehia, Wilaya na Mkoa. Aeleze mwaka uliojengwa Msikiti, waliojenga msikiti kamani Mfadhili au waumini wenyewe. Ainishe kama msikiti unasaliwa Ijumaa au hausaliwi Ijumaa.
Pia aeleze wastani wa watu wanao Sali katiak Msikiti huo, na sehemu ya kusalia wanawake imo au haimo katika msikiti.
Na mwisho utajwe uongozi wa Msikiti kwa majina yao pamoja na namba zao za simu kama ifuatavyo:-
Barua hii ya ombi la usajili wa Msikiti ipitie kwa Sheha wa Shehia uliopo Msikiti huo na Sheha atoe barua ya ombi la usajili wa Msikiti yenye anuani ifuatayo.
Katibu wa Mufti,
Ofisi ya Mufti
P.O.Box 2479
Zanzibar.
Barua zote mbili ziletwe ofisi ya Mufti kwa kuomba kusajili Msikiti.
USAJILI WA MADRASA
Katika kusajili madrasa unafuata utaratibu kama ulioelezwa katika usajili wa misikiti ispokua usajili wa Madrasa utaengeza mambo ya fuatayo.
Hatua au jinsi ya utaratibu wa Kusilimisha wasiokuwa Waisilamu
Zinatolewa huduma kwa walio silimu na wale wanaotaka kusilimu bure. Huduma hii ni ambayo haicheleshwi hata kidogo. Ndani ya nusu saa mwenye kusilimu anakabidhiwa tarjisi yake ya kusilimu.
Utoaji na Uendeshaji wa Mafunzo ya Ndoa
Kwa vile ofisi ya Mufti imejipanga vizuri sana. Masomo ya ndoa yanatolewa bure ndani ya muda wa meizi miwili na nusu kwa siku za Jumamosi na Jumapili tu, kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa sita mchana.
Fomu za mafunzo ya ndoa zinapatikana Ofisi ya Mufti bure, muhusika atajaza fomu ya mafunzo ya ndoa na kuirejesha ofisini. Na baada ya masomo vyeti vya uhitimu vinatolewa bure, ambavyo thamani yake ni kubwa mno katika jamii